RAIS DK. MWINYI ASHIRIKI MKUTANO WA SADC MJINI MAPUTO, MSUMBIJI AKIMWAKILISHA RAIS SAMIA.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa katika Mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wa Masuala ya Ulinzi na Usalama wa Nchi za Jumuiya hiyo, uliofanyika Maputo Nchini Msumbiji. Katika Mkutano huo ambao umeongozwa na Mwenyekiti wa SADC Rais wa Msumbuji Fellipe Jacinto Nyusi, Rais Mwinyi amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. (Picha na Ikulu)
Post a Comment