Featured

    Featured Posts

WAZIRI MKUU KUANZA ZIARA YA SIKU NNE KIGOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajia kuwasili mkoani Kigoma Februari 16, 2019 kwa ziara ya kikazi ya siku nne.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Emanuel Maganga amesema Majaliwa atatembelea wilaya ya Kigoma, Uvinza, Kibondo na Kakonko.

Amesema lengo la ziara yake hiyo ni kuweka mkazo na msisitizo katika ufufuaji na uendelezaji wa zao la chikichi ikiwa ni pamoja na  kukagua vitalu, mashamba, lengo likiwa ni uboreshaji wa zao hilo.

Amesema akiwa mkoani humo Waziri Mkuu atatembelea kambi ya wakimbizi ya Nduta iliyopo wilayani Kibondo na kuzungumza na wakimbizi.

Amebainisha kuwa pamoja na mambo mengine ataangalia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 ya CCM na kukagua miradi mbalimbali pamoja na kuzungumza na wananchi katika maeneo atakayokuwa anakutana nao.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana