Featured

    Featured Posts

RAIS MAGUFULI: ASKARI WP 4160 APANDISHWE CHEO

  Rais Magufuli ameagiza WP 4160 Beatrice Kayuni Mlanzi, kupandishwa cheo kutoka Koplo na kuwa Sajenti baada ya kuonesha utimilifu katika kazi.

Agizo hilo amelitoa jana Septemba 10, 2019, baada ya kupita katika kituo cha Polisi Selander Bridge.

Rais Magufuli alipita kituoni hapo akiwa njiani kurejea Ikulu, akitokea Taasisi ya Mifupa ya MOI katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokwenda kumjulia hali Baba Askofu Mkuu Ruwa'ichi.

Rais alimjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya MOI mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa Kichwa.
tangazo
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © 2025 Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana