Featured

    Featured Posts

CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU AFRIKA MASHARIKI CHANDINDULIWA UGANDA

Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Dkt. Aziz Ponary Mlima akizungumza wakati wa uzinduzi wa Chama cha wanafunzi wa Kiswahili Vyuo Vikuu Afrika Mashariki (CHAWAKAMA), uliofanyika jana tarehe 30 Novemba 2019, katika Chuo Kikuu Cha Ndejje, kilichopo Luwero nchini Uganda.

Tukio hilo lilihudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria wa Uganda,  Jenerali Kahinda Otafiire, Jenerali Salim Saleh, Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo Prof. Semakula Kiwanuka, Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Eriabu Lugujjo. Zoezi hilo pia lilihudhuriwa na Prof Aldin Mutembei kutoka Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam. 

Katika hotuba ya aliyoitoa Balozi Aziz P. Mlima, alizungumzia mchango wa Mwalimu Julius Nyerere kwa harakati za ukombozi wa Afrika kusini na Uganda na mchango wa Kiswahili kwa umoja wa kitaifa.

Prof. Aldin Mutembei alizingumzia maendeleo ya lugha ya Kiswahili kama moja ya lugha adhimu katika umoja wa nchi za kiafrika na jinsi kiswahili kinavyoweza kutumika bila kudhoofisha lugha zingine za kiasili. 

Jenerali Kahinda Otafiire alimwakilisha Rais Yoweri Museveni kwenye mdahalo huo.

Wanafunzi na uongozi wa Chawakama kutoka Chuo Kikuu cha Makerere walishiriki katika uzinduzi na mdahalo huo.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana