Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku

Magazeti ya leo, gazeti la mwananchi, global publisher, habari leo, habari mpya, ippmedia,magazeti ya leo tanzania, magazeti ya udaku, michuzi, michuzi blog, mpekuzi huru, mwananchi, mwanaspoti,nipashe, sekretarieti ya ajira

MENU
  • HOME
  • Drop Down 1
    • Element 1
    • Element 2
    • Element 3
  • Option 1
  • Option 2
  • Drop Down 2
    • Element 1
    • Element 2
    • Element 3
    • Element 4
  • Contact Us
Featured

    Featured Posts

*NAIBU SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA AWAPA FARAJA MAAFISA USAFIRISHAJI STENDI YA MBEYA

on 28/01/2020 Brown Alex
 
 
 
Na Maiko Luoga Mbeya

Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson Januari 21, 2020 alifanya ziara ya Kikazi katika kituo kikuu cha Mabasi mkoani Mbeya kwa lengo kutimiza ahadi yake ya kuwapatia Sare maalumu za kuwatambulisha maafisa usafirishaji katika jiji la Mbeya.

Maafisa hao maarufu kama Wapigadebe, wamepewa Sare hizo ili kuwaepusha na kero za kukamatwa mara kwa mara na Askari wa Jiji la Mbeya wakiwa hawana utambulisho maalumu wa kazi wanazozifanya wawapo kwenye Majukumu yao.

Aidha Dkt. Tulia amejionea na kuelezwa Changamoto mbalimbali zilizopo katika kituo hicho kikuu cha Mabasi ikiwemo ukosefu wa maji, ubovu wa miundombinu ya vyoo, uhaba wa taa kwaajili ya mwanga Majira ya usiku pamoja na Runinga maalumu ya kuwawezesha kufuatilia Taarifa na Matukio mbalimbali ya Kitaifa.

Changamoto nyingine ni pamoja na Ukosefu wa Vitendea kazi vya kubebea Mizigo ndani ya Stendi ikiwemo Toroli huku wakimuomba Naibu Spika Dkt, Tulia Ackson kuwawezesha upatikanaji wa mikopo kupitia Taasisi yake ya Tulia Trust.

Baada ya kuzungumza nao Dkt. Tulia ameahidi kushirikiana na Maafisa hao katika kutatua changamoto hizo huku akiwakabidhi Toroli moja la kubebea mizigo, kununua Taa za kufunga maeneo yanayozunguka kituo hicho cha Mabasi na kueleza kuwa atafanya jitihada za kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa haraka Kituoni hapo.

“Ndugu zangu niseme tu kwamba nimezisikiliza changamoto zenu na sisi kama Tulia Trust tunaahidi kushirikiana na Serikali yetu inayoongozwa na Rais Dkt, John Pombe Magufuli kuhakikisha tunawakomboa vijana katika janga la umasikini, na hata hili suala la mikopo vijana wa Tulia Trust watakuja hapa na kuwapa huduma”-Alisema Dkt, Tulia Ackson Naibu Spika.






  • email
  • facebook
  • linkedin
  • twitter
  • reddit
  • google+
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!
  • Rss
  • Twitter
  • FaceBook
  • Google +

Post a Comment

« Newer Posts Older Posts »

Popular Posts

  • MSIGWA AELEZA UMUHIMU WAHARIRI WA HABARI, TAASISI ZA UMMA KUKUTANA.
     Na Mwandishi Wetu Dodoma MSEMAJI Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Gerson Msigwa amesema kuna umuhimu wa wahar...
  • PICHA: UFUNGUZI WA MAFUNZO YA SIKU MBILI YA MITAALA ILIYOBORESHWA YALIYOANZA LEO KATIKA CHUO CHA UALIMU, MOROGORO
    Naibu katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dk. Frankilin Rwezimula, akifungua mafunzo ya Mtaala ulioboreshwa yaliyokuwa mahusu...
  • BALOZI DK. NCHIMBI ALIVYODHIHIRISHA KUWA MWANADIPLOMASIA ALIYEIVA, AWAPA 'AKILI' CHADEMA WASITUMIE MIGUU KUJENGA HOJA, WAJITOFAUTISHE NA MASHINDANO YA UREMBO AMBAYO NYENZO KUU NI UHODARI WA KUTEMBEA
    Na Bashir Nkoromo, CCM Official CCM Blog, Dar es Salaam Akizungumza katika mkutano wa mapokezi yake yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi ...

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Back To Top
Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana