Featured

    Featured Posts

CORONA: WATU WENGI WAKO MAJUMBANINA KUFANYA MTIKISIKO WA ARDHINI KUPUNGUA

Empty streets in Paris

Haki miliki ya pichaGETTY
Image captionMiji kote duniani haina watu kwasababu ya amri ya kusalia ndani kukabiliana na virusi vya corona
Mabilioni ya watu kote duniani kwasasa wanasalia nyumbani kwasababu ya virusi vya Corona - jambo ambalo linabadilisha mwenendo wa dunia.
Kwasababu ya amri ya kutotoka nje wanaokwenda kazini ama kutumia usafiri wa reli au wa barabara ni kidogo mno huku kampuni nyingi zikiwa zimefungwa.
Ukweli ni kwamba, idadi kubwa ya watu wanafanyakazi kidogo tu kuliko vile inavyotarajiwa na hilo limepunguza mitikisiko katika tabaka la juu la dunia.
Hii ni habari njema hasa ukizingatia kwamba dunia ina uzito wa tani trilioni bilioni sita.

Kupungua kwa kiasi kikubwa

Wanasayansi nchini Ubelgiji walikuwa wa kwanza kubaini hili, na kusema kwamba mitikiso ya ardhini imepunga sana tangu kuanzishwa kwa hatua za amri ya kutotoka nje katika baadhi ya mataifa duniani.
Mabadiliko hayo pia yametambuliwa katika maeneo mengine duniani.
Coronavirus
Banner
Mtaalamu mmoja wa masuala ya matetemeko ya ardhi, mfanyakazi katika Taasisi moja ya masuala ya ardhini amesema mitikiso ya ardhini katika mji mkuu wa Ufaransa umepungua sana, huku Marekani mitikiso hiyo ikisemekana kupungua hata zaidi kulingana na utafiti wa chuo kikuu cha Cal Tech.

Hali safi ya hewa na bahari tulivu

Hii sio njia pekee ambayo virusi vya corona vimebadilisha maisha ya kila siku kote duniani.
Setilaiti zimebaini kupungua kwa uchafuzi wa mazingira kunakosababishwa na gesi ya naitrojeni dioksaidi, ambayo chanzo chake ni magari, malori, mabasi na viwanda vya kuzalisha umeme.
A person wearing a mask walks in front of a large cruise shipHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMlipuko wa janga la corona umesababisha usafiri wa meli kusitishwa katika maeneo mengi na kufanya bahari kuwa tulivu
Dunia imenyamaza mno.
Mwanasayansi ambaye hupima kiwango cha kelele katika miji mbalimbali kila siku na wale watafiti wa kina cha bahari wanasema kwamba kiwango cha sauti kimepungua.

Mawimbi mazuri

Utafiti mpya wa matetemeko ya ardhi hakumaanishi kwamba dunia imeacha kutikisika kabisa, lakini mabadiliko hayo siyo tu kwamba yanashuhudiwa na wanasayansi lakini pia ni muhimu sana kiuhalisia.
Shughuli za binadamu ni kama kelele za chinichini ambako kunafanya iwe vigumu zaidi kusikiliza uhalisia wa kinachokea ardhini.
An image of Earth taken from spaceHaki miliki ya pichaGETTY
Image captionTabaka la juu la dunia linaweza kuwa na unene wa mita hadi 70000, lakini bado hutikisika kwasababu ya shughuli za mwanadamu
“Utapata ishara ambayo haina kelele sana ambayo inawezesha kupata taarifa kidogo,” mtaalamu wa matetemeko Andy Frassetto kupitia mtandao, ameelezea katika Taasisi za Utafiti wa matetemeko ya ardhi mjini Washington.
Baadhi ya watafiti wamefanikiwa kuzungumzia kile hasa kile kinachosababisha kupungua kwa mitikiso ya chini ya ardhi.
Stephen Hicks, kutoka chuo cha Imperial College London, amesema kwamba kupungua kwa mitikiso ya chini ya ardhi katika eneo lake kumetokana na kupungua kwa msongamano wa magari kati ya London na Wales.
“Ni wazi kwamba katika siku chache zilizopita, kiwango cha kelele alfajiri kimepungua kuliko siku za nyuma,” ameandika kwenye mtandao wa Twitter.
Nadhani hili ni kwasababu hakuna tena msongomano wakati wa asubuhi huku idadi ndogo tu ya watu ikiwa ndo inayoabiri usafii uliopo na shule pia zimefungwa.”

Mabadikilo ya muda

Mabadiliko haya yana chanzo chake.
Bila shaka shughuli za binadamu hutofautiana kila siku kwasababu pia kuna wakati ambao shughuli hupungua.
Usiku huwa ni tulivu ikilinganishwa na mchana na kupungua kwa mitikiso namna hii hutokea wakati wa sikukuu kubwa au matamasha.
Lakini kile kinachotokea kote duniani ni kupungua kwa shughuli kwa wiki kadhaa, au miezi tukio ambalo hushuhudiwa wakati wa sikuu ya Krismasi katika nchi za Kikiristo.

Mada zinazohusiana

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana