Featured

    Featured Posts

  Idadi ya wagonjwa wa virusi vya coronavirus nchini Kenya  sasa imefikia 234 baada ya watu 9 zaidi kuthibitishwa kuambukizwa ugonjwa huo.

Hayo ni kwa mujibu wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye amelihutubia taifa hilo leo Alhamisi  April 16 akiwa Ikulu ya Nchi hiyo.

Kenyatta amesema kwamba serikali ilipima sampuli zingine 704 kwa muda wa saa 24 zilizopita na ndipo hao  watu  tisa wakathibitishwa kuugua. 

Uhuru pia amesema idadi ya watu 53 wamepona kabisa na kuruhusiwa kwenda nyumbani tangu janga hili lilipotangazwa kuingia nchini humo

Aidha ametangaza kuwa watu 11 wamepoteza maisha yao, wengine 1,000 wakisalia karantini na wengine 156 wakitengwa katika sehemu mbalimbali nchini humo.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana