Featured

    Featured Posts

MTOTO WA MIAKA 17 MIKONONI MWA POLISI KWA KWA TUHUMA ZA KUMUUA BABA YAKE

 Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linamshikilia mtoto wa miaka 17 kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa  Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, alidai kuwa Mei 31, saa 12 alfajiri Kitongoji cha Manyani, Kata ya Mkalama wilayani Gairo, mtu aliyejulikana kwa jina la Issaya Lameck (41), maarufu kama Kusaganika, fundi Muwashi, aliuawa kwa kupigwa na mtoto wake mwenye miaka 17 (jina linahifadhiwa kwa sababu za kimaadili).

Kamanda Mutafungwa alisema siku ya tukio hilo, Issaya alirudi nyumbani akiwa amelewa, ndipo ulipozuka ugomvi ambapo mtoto wake anadaiwa alimpiga ngumi sehemu za usoni na alipodondoka chini aliendelea kumkanyaga sehemu za tumboni hali iliyosababisha kupata maumivu makali.

Alisema baada ya tukio hilo, ndugu wa Kusaganika walioamulia ugomvi huo, hawakuweza kumpatia msaada wa kimatibabu kutokana na hali ya ulevi aliyokuwa nayo wakati wa tukio.

Kwamba pamoja na mwenyewe kudai hajaumia, lakini ilipofika saa 12 alizidiwa na kufariki dunia.

Kamanda Mutafungwa alisema mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na daktari na kwamba umekabidhiwa ndugu kwa taratibu za mazishi.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana