Featured

    Featured Posts

NMB YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SH. MIL. 40 DODOMA, UZINDUZI WA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA+video

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka (katikati) akipokea kutoka kwa Afisa  Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna msaada wa  mashuka na vitanda kwa ajili ya kutumika katika baadhi ya hospitali za mkoa huo. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda.

Katika tukio hilo NMB imetoa msaada wa vitanda, mashuka, mabati na madawati vyote vikiwa na thamani ya sh. mil. 40.

Makabidhiano hayo zamefanyika wakati wa uzinduzi wa  Wiki ya Kimataifa ya Huduma kwa Wateja wa NMB, jijini Dodoma leo Oktoba 4, 2021.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mtaka msaada wa madawati kwa ajili ya shule  mkoani humo.
Mkuu wa mkoa Dodoma, Mtaka akipokea msaada wa mabati kwa ajili ya kuezekea vyumba vya madarasa katika baadhi ya shule mkoani humo.
Mtaka akizindua Hati ya kiapo cha huduma kwa wateja wa NMB
Mtaka akiwakabidhi yawadi ya vyeti baadhi ya wateja wa benki hiyo na wafanyakazi bora wa benki hiyo.











Mbunge wa Dodoma  Mjini, Anthony Mavunde akitoa pongezi kwa NMB kwa misaada mbalimbali wanayotoa katika sekta ya elimu jimboni humo.
Mbunge wa Bahi, Nollo akiishukuru NMB kwa msaada waliotoa wa mabati, mashuka na vitanda lakini vile vle kumpatia yeye mkopo wa fedha ya kuendeshea biashara yake.


Mkurugenzi wa Kampuni ya Royal Agri,  akitoa pongezi kwa NMB kwa kumpatia mkopo pamoja na kutoa mikopo kwa vijana.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Jabir Shekimweri akitoa shukrani kwa NMB kumpatia mkopo uliomfanya anunue basi na hivi sasa ana mabasi mengi.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, akitoa pongezi kwa NMB kwa kuipatia wilaya hiyo misaada ya hali na mali.
Mkuu wa Wilaya ya Bahi,  ambaye pia ni Mwenyekiti wa wakuu wa wilaya nchini, Mwanahamisi Munkunda akitoa shukrani kwa NMB kuwa karibu nao  kwa kutoa misaada katika wilaya mbalimbali nchini.



Mteja wa NMB, Jane Kiroma wa kampuni ya RJ akitoa pongezi kwa Benki ya NMB kwa kumpatia mkopo uliosaidia kuanzisha kampuni hiyo.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA




Madau, nakuomba uendelee kusikilza kupitia clip hii ya video kujua yaliyojiri wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja......
Imeandaliwa na Richard Mwaikenda
 Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
 0754264203
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana