Featured

    Featured Posts

KASINO NDANI YA MWANZA HOTELI YATEKETEA

 


  Kasino iliyopo Mwanza  Hotel  jijini Mwanza imeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijafahamika

Inaelezwea kuwa hakuna hakuna mtu aliyedhurika na moto huo  japo umesababisha hasara katika kasino hiyo kwa kuteketeza vitu vyote vilivyokuwa ndani


Jeshi la zimamoto na uokoaji lilifika kwa wakati na kuanza kuuzima moto huo ili usiendelee kuleta madhara kufuatia hoteli hiyo kuwa katikati ya jiji la Mwanza na kuzungukwa na majengo mengine 


Miongoni mwa waliofika katika tukio hilo ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Adam Malima 


Kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Kamila Labani amesema wamefanikiwa kuudhibiti moto huo usisambae katika hoteli hiyo huku bado wanaendelea kuchunguza chanzo cha moto huo

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana