Featured

    Featured Posts

WAZIRI BITEKO AIPONGEZA GF TRUCKS & EQUIPMENTS LTD KWA KUJALI AFYA ZA WANANCHI

Na mwandishi Maalum, Geita

Waziri wa madini  amewataka wananchi na wakazi wa Geita kujenga  tabia ya kujitolea kuchangia Damu ili kusaidia Majerui wa ajali mbali mbali.


Waziri  aliyasema hayo wakati akikagua maonyesho ya madini na kutembelea katika banda la kampuni ya  GF Trucks & Equipment’s  ndani ya  Maonyesho hayo na kukuta zoezi la uchangiaji Damu  wa  hiari lilkiendelea chini ya  Kitengo cha Damu salama  kwa kushirikiana na kampuni ya GF  Trucks & Equipments Ltd


Kampuni hiyo iliweza kuhamasisha wadau mabali mbali wakiwemo madereva Boda boda na Bajaji katika mkoa wa Geita na kuweza kushiriki uchangiaji Damu kwa hiari na  jumla ya chupa 25 za damu ziliweza kupatikana katika zoezi hili.


Nae  Dereva Bajaji, Martini Malima alisema alikua anaogopa kutoa damu kwa kuhofia usalama wake lakini baada ya watu wa kampuni ya GF Trucks & Equipment’s  kumhamasisha ameweza kuchangia damu ambayo itawasaidia watu waopata ajali lakini wakikosa ndugu wa kuwasaidia basi damu hii itatumiaka kuokoa maisha yao


Kwa upande wake Meneja  Masoko  na mawasilioano wa kampuni ya GF , Smart  Deusi alisema kampuni hiyo imeweza kuratibu zoezi hilo kutokana na wao kuwa wauzaji wa magari na mitambo na kwa kuziongatia ajali nyingi zinazotokea barabarani tukaamua kuwashawiwhi watu wa bodabooda na bajaji kushiriki zoezi hili.


GF  Tumeamua kufanya hivi ikiwa ni sehemu ya kurejesha kwa jamii  faida tunayoipata ikiwamo kuisaidia serikali katika kunusuru wahanga wa ajali kwa kuchangisha Damu na tunashukuru tumefanikiwa kupata chupa 25


Hii ni mara ya tatu tunaratibu zoezi la uchangiaji damu na pia kwa kanda ya ziwa tumekuwa wadhamini wa mpira kwa timu ya Mbao hapo awali na sasa ni sahemu ya wadhamini wa Timu ya Geita inayoshiriki Ligi kuu.


Pia kampuni hiyo imeshiriki maonyesho ya madini ikiwa na lengo la kuwasogezea bidhaa wadau wa sekta ya madini ikiwamo Tipper aina ya FAW pamoja na mitambo ya kichimbia madini ya XCMG ambavyo vinapatikana katika banda la kampuni hiyo Pia kuna offa kwa wateja wa mwazo wazawa ambao watanunua mashine pamoja na magari katika kindi hiki cha maonyesho

Waziri wa Madini, Dotto Biteko  akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd wakati wa maonyesho ya Madini  yanayoendelea mkoani Geita.

Waziri wa Madin, Dotto Biteko akipata maelekezo kutoka kwa Afisa mauzo wa  Kampuni ya GF Trucks &Equipments Ltd, Poul Msuku wakati alipotembelea banda lao kwenye Maonyesho ya Madini mkoani Geita.
 Kijana akichangia damu
Maofisa wa Dam salama wakihifadhi chupa za damu. (Picha zote na Said Khamis)
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana