Wanawake kutoka mikoa mbalimbali wakicheza kwa furaha wakati wa mkutano wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), kumpongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ushindi mkubwa alioupata wa uenyekiti na kutunukiwa shahada ya udaktari.
Mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Novemba 9, 2022 jijini Dodoma umempongeza pia Mwenyekiti mpya wa UWT, Mary Chatanda na MAkamu Mwenyekiti, Zainab Shomari.
Mwenyekiti mpya wa UWT, Mary Chatanda (kulia)na Makamu Mwenyekiti, Zainab Shomari. |
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma, Neema Majule akisalimia kabla ya kutoa salamu za pongezi za mkoa huo kwa Rais Samia na Mary Chatanda.
Mmoja wa waasisi wa UWT, Getrude Mongela akiwafunda viongozi na wanawake kwa ujumla.
Post a Comment