Featured

    Featured Posts

LUDIGIJA ATAMBA HAKUNA MTOTO ATAKAYEKOSA KUSOMA DAR KWA UHABA WA MADARASA

Na Christopher Lissa

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ludigija, amesema hakuna mtoto aliyechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza atakayekosa nafasi kutokana na kukosa darasa.


Shule  zinatarajiwa kufunguliwa keshokutwa nchini kote, Ludigija amewataka wazazi na walezi kuhakikisha kila mtoto aliyechaguliwa anaripoti shuleni. 


Alitoa mwito huo, alipokuwa akipokea madarasa 310 yaliyojengwa kwa Sh. Bilioni6.3 zilizotolewa na Rais Dk. Samia  Suluhu Hassan.


Katika hafla hiyo iliyofanyika Shule ya Sekondari Nguvu Kazi, Kata ya Chanika, Ludigija alisema, Rais Dk. Samia, alitoa fedha hizo kujenga madarasa 310 katika Halmashauri ya Jiji  la Dar es Salaam.


Alisema kwa mkoa mzima wa Dar es Salaam, Rais Dk. Samia alitoa kiasi cha sh. bilioni 12 kujenga madarasa.


“Ilala tulipata nusu ya fedha hizo yaani sh.  bilioni 6.2. Tumefanikiwa kujenga madarasa 273  ya msambao na yaliyosalia tuna jenga ghorofa,”alisema  Ludigija.

DC Ludigija (kushoto) akitoka kukagua madarasa wakati wa hafla hiyo.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana