Featured

    Featured Posts

GAVANA WA NAIROBI, MIKE SONKO ATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA UHALIFU WA KIUCHUMI

     
     
  •  
Sonko anayefahamika sana kwa kuvalia vito vya dhahabu anajiunga katika safu ya  maafisa wengine kadhaa wa ngazi ya juu wa serikali akiwemo Waziri wa Fedha Henry Rotich ambao hivi karibuni walihusishwa na tuhuma hizo za ufisadi na ulaji rushwa. Kamata kamata hii inatajwa kuwa ni katika juhudi za serikali ya Kenya za kupambana na ufisadi nchini.
Yassin Amaro msemaji wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi ya Kenya (EACC) amesema kuwa gavana wa Nairobi ametiwa mbaroni na maafisa wao huko Voi na kusafirishwa hadi Nairobi.
Gavana wa Nairobi akirejeshwa Nairobi kwa helikopta 
baada ya kukamatwa huko Voi 

 
Gavana huyo wa Nairobi na maafisa wengine wa kaunti hiyo wanatuhumiwa na Noordin Haji Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka wa serikali kwamba wameinufaisha na manunuzi yasiyo ya kawaida na malipo ya kiasi cha shilingi milioni 375 za kaunti hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka wa Kenya (DPP) amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha wa kumshtaki Sonko na maafisa wengine wa kaunti ya Nairobi kwa kujipatia kinyume cha sheria mali za umma, kutakatisha fedha na jinai nyingine za kiuchumi.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © 2025 Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana