Featured

    Featured Posts

MBUNGE WA IRAQ: MAANDAMANO YA IJUMAA NI KURA YA MAONI YA KUONDOA ASKARI WA MAREKANI

Mohammad  al Baldawi, amesema kuwa, maandamano yaliyopangwa kufanyika kesho Ijumaa kote Iraq yatabainisha wazi msimamo wa wananchi kuhusu uwepo wa wanajeshi wa Marekani katika ardhi ya Iraq. Ameongeza kuwa: "Jitihada za Marekani za kuendelea kubakia kijeshi Iraq zimefeli."
Kesho Ijumaa 24 Januari wananchi wa Iraq wanatazamiwa kujitokeza kwa wingi katika miji mbali mbali ya nchi hiyo baada ya Sala ya Ijumaa kushiriki katika maandamano yaliyo dhidi ya Marekani. Viongozi wa kisiasa, kidini na kitaifa nchini Iraq wametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maandamano hayo ya kihistoria.
Bunge la Iraq
Kufuatia hujuma ya kigaidi ya Marekani ya Januari 3 iliyopelekea kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu na Abu Mahdi al Muhandis, Naibu Kamanda wa Kikosi cha Kujitolea cha Wananchi wa Iraq (Al Hashd al Shaabi) na wenzao wanane, Bunge la Iraq mnamo Januari 5 lilipitisha kwa kauli moja muswada wa kutaka wanajeshi wa Marekani waondoke nchini humo.
Viongozi wengi wa Iraq akiwemo Waziri Mkuu Adel Abdul Mahdi, wameunga mkono uamuzi huo wa bunge na wanasisitiza kuwa wanajeshi wa Marekani wanapasa kuondoka Iraq mara moja.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana