Featured

    Featured Posts

MEYA IRINGA ANG'OLEWA

  Baraza la Madiwani la Manispaa ya Iringa limemwondoa Meya wa Manispaa ya iringa-Chadema Alex Kimbe baada ya kupiga kura ya kutokuwa na imani nae kufuatia tuhuma mbalimbali za matumizi mabaya ya madaraka


Kimbe ambaye anatokana na chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema ameng’olewa madarakani leo Jumamosi Machi 28, 2020 katika kikao maalum cha madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa hiyo.

Akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa, mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa, Joseph Ryata amesema wajumbe waliohudhuria kikao ni 26 na kura 14 zimeridhia kumuondoa meya huyo.

Miongoni mwa tuhuma ambazo alikuwa anakabiliwa nazo Kimbe ni matumizi mabaya ya madaraka ikiwamo kufanya uamuzi bila kuzingatia kanuni za kudumu za Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana