Featured

    Featured Posts

IDADI YA MAAMBUKIZO CORONA NCHINI MREKANI YAFIKIA LAKI SABA


Takwimu za hivi punde zinaonyesha kuwa, watu 710,272 wameambukizwa virusi vya Corona nchini Marekani huku 37,175 wakiaga dunia na kuifanya nchi hiyo kuwa ndio iliyoathiriwa zaidi na virusi hivyo duniani.

Italia inashika nafasi ya pili kwa idadi kubwa ya watu walioaga dunia kwa virusi vya Corona ambapo hadi sasa watu 22,745 wamefariki dunia nchini humo, ingawa kwa upande wa idadi ya maambukizo inashika nafasi ya tatu. 

Uhispania yenye idadi 20,002 ya vifo vya Corona, jumla ya watu 190,839 wameambukizwa virusi vya Corona katika nchi hiyo ya bara la Ulaya.

Nchi zinazofuata ni Ufaransa, Ujerumani na Uingereza na kulifanya bara la Ulaya kwa sasa kuwa kitovu cha virusi vya Corona.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana