Featured

    Featured Posts

WHO: AFRIKA HUENDA IKAATHIRIKA ZAIDI NA VIRUSI VYA CORONA

  Shirika la Afya Duniani, WHO, limeonya kwamba bara la Afrika huenda likawa na idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Corona. 


WHO inabashiri kuwa hali ikiendelea ilivyo sasa, huenda idadi ya vifo ikafikia 300,000 na watu wengine zaidi ya Milioni 30 kuwa masikini.

Kufikia sasa Afrika ina vifo karibu elfu moja vinavyohusishwa na Corona, huku watu zaidi ya elfu 19 wakiambukizwa ugonjwa huo.

Wakati huo huo Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, limetaka Afrika isaidiwe kukabiliana na ugonjwa hatari wa Covid-19.

IMF imetoa wito wa msaada wa haraka wa kimataifa kwa nchi za Afrika ambazo zinakabiliwa na janga hilo.

Mkurugenzi mkuu wa IMF Kristalina Georgieva amewaambia mawaziri, maafisa wa Umoja wa Mataifa na wengine kwamba bara la Afrika halina raslimali za kutosha na miundo mbinu ya kutosha ya afya ili kukabiliana na janga hilo na kwamba linahitaji karibu dola bilioni 114.

Maambukizi ya virusi vya Corona kote ulimwenguni sasa yamepindukia milioni 2.18 na watu 150,000 wamepoteza maisha.
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana