Rais Yoweri Museveni aamua kutoa mfano wa jinsi mtu anaweza kufanya mazoezi akiwa nyumbani na kubaki salama wakati huu ambako kuna maambukizi ya virusi vya corona.
Video inayomuonyesha Museveni mwenye umri wa miaka 75 akipiga 'push up' arobaini huku sauti ya mtoto ikisikika kuhesabu, imeibua gumzo mtandaoni wakidai kuwa rais huyo bado ana nguvu.
Hii ni mara ya pili kwa rais Museveni kuonyesha video akiwa anafanya mazoezi, mwezi Aprili alitoa video ya namna hiyo wakati wa marufuku ya kutoka nje ambayo iliisha mwezi Juni.
Uganda inatarajia kuwa na uchaguzi Januari 2021 na kupiga marufuku wagombea kufanya mikutano ya hadhara huku akitaka watu kutumia radio na TV.
Post a Comment