Featured

    Featured Posts

LUKUVI, ASAS WAONGOZA WANANCHI KUMLAKI DK MAGUFULI ISIMANI, IRINGA

 

Mgombea ubunge  wa jimbo la Isimani mkoani Iringa Mh. William Lukuvi na MNEC wa mkoa wa Iringa Bw. Salim Abri Asas wakiwapungia mikono wananchi wa Migori waliojitokeza kumlaki Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM wakati alipopokelewa mkoani humo katika mji wa Migori.

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na Mwenyekiti wa chama Rais Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Migori jimbo la Isimani  mkoani Iringa baada ya kuwasili njiani kuelekea  Iringa mjini ambako atahutubia mkutano mkubwa wa kampeni leo Jumatatu Septemba 28, 2020.

Mgombea ubunge  wa jimbo la Isimani mkoani Iringa Mh. William Lukuvi na MNEC wa mkoa wa Iringa Bw. Salim Abri Asas wakipiga makofi wakati  Mgombea wa Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli alipopokelewa mkoani humo katika mji wa Migori.

Mgombea ubunge  wa jimbo la Isimani mkoani Iringa Mh. William Lukuvi akimuombea kura mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM Rais Dk. John Pombe Magufuli wakati alipowasili katika mji wa Migori mkoani Iringa.

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi kulia na Mkuu wa wilaya ya Iringa mjini Richard Kasesela wakimsikiliza mgombea Urais wa Tanzania kupitia (CCM) Dk. John Pombe Magufuli wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Migori mkoani Iringa.

Picha mbalimbali zikionesha maelfu ya wananchi waliojitokeza kumlaki mgombea Urais wa Tanzania kupitia (CCM) Dk. John Pombe Magufuli wakati alipowasili katika mji wa Migori mkoani Iringa.

  

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana