Featured

    Featured Posts

MBIONI KEMONDO MKOANI KAGERA KUPATA MAJI SAFI NA SALAMA

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba akiwa katika kikao kuhusu mwitikio wa wananchi kuhusu mradi wa maji wa Kemondo na Burhan Mohammed, Mtendaji wa Kijiji cha Rwagati (katikati) na Cyriacus Sosthenes, Mtendaji wa Kata ya Kemondo (kulia). Kushoto ni Mhandisi Lyidia Joseph, Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Huduma ya Maji wa Wizara ya Maji.
Mfanyabiashara ya Samaki, katika kambi ya mabanda ya uvuvi-Kemondo,  Bi. Christina Wangwi,  akitoa maoni yake kuhusu mradi wa maji wa Kemondo ambapo ametoa maoni ya kuongezewa  muda zaidi  kuwezesha kuhamisha vifaa katika eneo la ujenzi wa chanzo cha maji na kuhamia katika eneo mmbadala ambalo limeshaandaliwa kwa shughuli hiyo ya kuuza samaki.

Baadhi ya wajasiriamali wa samaki katika kambi ya uvuvi  ya Kemondo wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba (Hayupo pichani), katika kikao kifupi alichopokea maoni yao kuhusu mradi wa maji wa Kemondo
Ujenzi wa mabanda ukiendelea katika eneo jipya lililoandaliwa kwa ajili ya mabanda ya kambi ya uvuvi Kemondo. Eneo jipya limeanzishwa ili kupisha utekelezaji wa mradi wa maji na kuepuka uchafuzi wa maji kuzunguka eneo la chanzo
 
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana