Featured

    Featured Posts

DODOMA IPO SALAMA WAGENI KARIBUNI SIKU YA KUAPISHWA KWA RAIS-MUROTO


…………………………………………………………………..

Na.Alex Sonna,Dodoma

Kamanda wa  Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu kuwapokea wageni wote wanaotarajiwa kufika katika hafla ya  sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule Dk John Magufuli zilizopangwa kufanyika Novemba 5,2020 kwenye uwanja wa Jamuhuri jijini Dodoma.

Pia Kamanda Muroto ametoa onyo kali kwa watu watakaoandamana kuingia barabarani bila kufuata taratibu.

Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Muroto amesema kuwa mkoa wa Dodoma kiujumla upo salama kabisa hivyo wageni 
wote wanaotarajia kufika waje na wasiwe na wasiwasi. 

“Kwa ujumla jiji la Dodoma lipo salama kabisa  kila mmoja anafanya shughuli zake za maendeleo,napenda kuwaambia wageni wote wanaotarajia kuja katika hafla za kuapishwa kwa Rais Mteule waje wakiwa na amani jeshi la polisi lipo na limeweka ulinzi katika kila kona ya eneo,”amesema Muroto.

Muroto amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kila kona kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya jijini hapa.

Hata hivyo amesema kuwa kitu kinachoitwa maandamano haramu hakitakiwi barabarani, mtu akiingia barabarani inamaana anataka kulichokoza Jeshi la Polisi kutokana na kuwa kamanda Simon Sirro alishaeleza kuwa maandamano hayo ni haramu.

“Wale wamepigwa kwa kipigo cha mbwa kachoka kupitia kura za wananchi,Jeshi la Polisi litawapiga kwa kipigo cha mbwa koko kwa wale watakaojitokeza kufanya maandamano haramu,”amesema  Muroto.




 
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana