Featured

    Featured Posts

TAKUKURU KAGERA YANUSURU MWANAFUNZI DHIDI YA RUSHWA YA NGONO.

Na Lydia Lugakila

Bukoba:

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Kagera imemshikilia mkufunzi mmoja aliyetambulika kwa jina la Ruta Cleophace Kyaragaine mwenye umri wa miaka 59 kwa tuhuma za kumuomba rushwa ya ngono mwanafunzi.


Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari  mkuu wa Takukuru Mkoani Kagera John Joseph amesema mkufunzi huyo anashikiliwa kufuatia kupokewa kwa taarifa kutoka kwa mwanafunzi mmoja ambaye anasoma katika chuo hicho (jina lake kozi anayosoma vimehifadhiwa) kuwa mkufunzi huyo aliyejulikana kwa majina ya Ruta Cleophace Kyaragaine amekuwa akimuomba rushwa ya ngono mwanafunzi huyo tangu mwaka 2020 kwa madai ya kwamba atamsaidia ki masomo na kuwa endapo hatokubali kushiriki naye ki ngono basi hatomaliza masomo yake.


John Joseph amesema kuwa  kufuatia kupokewa kwa taarifa hiyo taasisi hiyo ilianza uchunguzi mara moja ambapo Aprili 3, 2021 maafisa hao walimkamata mkufunzi huyo katika nyumba ya kulala wageni iliyopo Manispaa ya Bukoba Mkoani humo akiwa na mwanafunzi huyo huku akilazimisha kupewa ngono na kutoa baadhi ya ahadi na vitisho kwa mwanafunzi huyo.


"Uchunguzi wa tuhuma hii uko katika hatua za mwisho na ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili aweze kujibu tuhuma hizo zinazomkabili" alisema Joseph.


Hata hivyo mkuu huyo wa Takukuru ametoa wito kwa wananchi Mkoani humo kutambua kwamba rushwa ya ngono ni rushwa inayotakiwa kupingwa kwa nguvu zote kwani hudhalilisha utu wa mwanamke na madhara yake ni makubwa muno.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana