Featured

    Featured Posts

MWAKANG'ATA ATAKA UJENZI UWANJA WA NDEGE SUMBAWANGA UANZE, BARABARA YA KIBAONI HADI MLOWO ITIWE LAMI+video

 Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa, Bupe Mwakang'ata ameishauri serikali kuharakisha malipo ya wakandarasi nchini ambao wanaidai serikali baada ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu nchini. 

 

Pia Mbunge Mwakang'ata ameiomba serikali kuanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Sumbawanga Mjini ambao umetelekezwa licha ya kulipa fidia walioupisha ujenzi. Aidha mbunge huyo ameiomba serikali kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Kibaoni-Majimoto hadi Mlowo kutokana na umuhimu wake kiuchumi. 

 

 Mwakanga'ata alitoa ushauri huo alipokuwa akichangia mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi wakati wa Mkutano wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kikao cha 30 jijini Dodoma Mei 18, 2021. 

 

Mdau nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Mbunge Mwakang'ata akitoa ushauri wake huo..... 

 

 

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana