Tegeta, Dar es Salaam, leo
Kanisa Halisi la Mungu Baba, limeandaa Ibada kubwa ya Sherehe ya kuzaliwa rasmi kwa Kanisa hilo na kwenda Mataifa Mengine, ambayo itafanyika siku ya Jumapili, Juni 6, 2021 (12 Abibu Vol. 2).
Taarifa iliyotolewa leo na Kiongozi Mkuu wa Kanisa hilo Baba Halisi, imesema, Ibada hiyo itafanyika siku hiyo ya Jumapili, Juni 6, 2021, kwenye Makao Makuu ya Kanisa hilo, Tegeta Kibo, Dar es Salaam, kuanzia saa 11 Alfajiri hadi saa 5 asubuhi.
Katika taarifa hiyo, Baba Halisi, amesema ibada hiyo itakuwa ya muhimu sana, na amewakaribisha watu wote bila ubaguzi wowote kuihudhuria.
Post a Comment