Featured

    Featured Posts

WAZIRI MHAGAMA: VYAMA VYA WAFANYAKAZI PAZENI SAUTI KUISHUKURU SERIKALI INAPOMWAGA AJIRA+video

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Jenista Mhagama amefungua mkutano wa pamoja na viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini jijini Dodoma Aprili 9, 2022 na kuwaeleza kuwa wanapaswa kupaza sauti kuishukuru Serikali inapotangaza ajira mpya za wafanyakzi kwani kwa upande wa vyama vinaongeza mapato na kuwa hai zaidi. Mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako (kulia) lengo lake lilikuwa ni kuelezea mtizamo wa Serikali ya Awamu ya Sita katika uimarishaji wa utumishi wa umma unaowajibika kwa hiari na matumizi ya mifumo ya Tehama katika utendaji na utoaji huduma bora katika utumishi wa umma.



Kaimu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Utumishi ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu  Xavier Daudi .   akitoa maneno ya utangulizi wakati wa mkutano huo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deo Ndejembi akimkaribisha Waziri Mhagama kufungua mkutano huo.
Viongozi wa vyama vya wafanyakazi wakifuatilia kwa makini wakati Waziri Mhagama akifungua mkutano huo.



Wanahabari wakisikiliza  wakati Waziri Mhagama akihutubia wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.

PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA

Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Waziri Mhagama na Waziri Ndalichako pamoja na Rais wa Shirikisho la Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Nyamhokya wakizungumzia kuhusu mkutano huo.....


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
 MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
 0754264203
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana