Hospital ya wilaya ya Same imetoa Elimu ya uhamasishaji na uchangiaji Damu salama kwa hiari lengo ni kusaidia wagonjwa ambao wanapungukiwa damu hasa wale wanaopata ajali na wamama wajawazito wakati wa kujifungua hili kupungaza vifo vinavyo tokana na upungufu wa Damu
Hayo yamesemwa na Mganga mkuu wa wilaya ya Same Doctor Alex kwenye Maadhimisho ya Uhuru wa miaka 61 ya Tanzania bara amewaomba watanzania kwa ujumla kuwa wazalendo na Taifa kwa kushirikiana kwa kudumisha Amani na umoja ni nguzo ya maendeleo yetu
Aidha Doctor Alex aliwaomba watumishi wote kwenye sekta ya Afya kuwa wazalendo kwenye kutoa huduma za matibabu kuepusha vifo vya kizembe kwa wagojwa
Aliendelea kusema serikali imejipanga kikamilifu kuakikisha kila kijiji kinapata kituo cha Afya cha kisasa na madawa ya kutosha lengo ni kuwataka wananchi wake wanapata huduma bora za matibabu na kufanya shughuli zao za kiuchumi na kulijenga Taifa
Post a Comment