Featured

    Featured Posts

WAFANYABIASHARA DODOMA WAPIGWA MSASA ANWANI ZA MAKAZI ZIKAVYOWANUFAISHA

 

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Aloyce Mwogofi akielezea umuhimu wa  anuani za makazi kwa wafanyabiashara alipokuwa akifungua mafunzo kwa wanayabiashara yaliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Mawasliano na Teknolojia ya Habari jijini Dodoma Disemba 13, 2022.
Mjumbe wa Timu ya Uratibu Mfumo wa Anuani za Makazi Kitaifa, Arnold Mkude akielezea muundo wa mfumo wa anuani za makazi na manufaa yake.
Mkurugenzi wa Huduma za Mawasiliano Wizara ya Habari, Mawasliano na Teknolojia ya Habari,  Mhandisi Clarence  Ichwekeleza akisema neno la utangulizi  kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi.
Mtaalamu wa Mfumo wa Kidijitali wa Anuani za Makazi,  Masele Mabula akielezea  kuhusu postikodi


Baadhi ya maafisa wa serikali.
Baadhi ya wafanyabiashara wakiwa katika mafunzo hayo





Baadhi ya Wanahabari wakiwa katika kikao hicho


PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA


Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imeeleza kuwa utekelezaji wa mfumo wa anwani za makazi nchini, unawezesha mipango na tafiti kufanyika kwa tija, kuongeza vyanzo vya fedha, kuimarisha usalama ,kuwezesha utoaji , upatikanaji na upelekaji  wa huduma za bidhaa hadi mahali husika.


Hayo yamebainishwa na Mjumbe wa Timu ya Uratibu Mfumo wa Anwani za Makazi Kitaifa, Arnold Mkude kwenye kikao kazi kati ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari na wafanyabiasha wa Jiji la Dodoma kuhusu umuhimu wa  utekelezaji wa mfumo wa anwani za makazi.


Ametaja manufaa mengine kuwa ni kusaidia wawekezaji kufanya uamuzi kabla ya  kufanya uwekezaji na  kuwezesha biashara mtandao kufanikiwa hali itakayo inua fursa ya uchumi wa kidigitali.


Pamoja na hayo alitumia nafasi hiyo kueleza muundo wa anwani za makazi kwa upande wa vijijini kuwa unahusisha namba ya nyumba au jengo, jina la kitongoji au shehia na namba maalumu ya postikodi na kwa upande wa Miji, muundo wa anwani za makazi unahusisha namba ya nyumba ,jina la mtaa au barabara,namba ya kata au postikodi.


"Jamii inapaswa kutambua kuwa postikodi ni utaratibu wa kitaalam unaotumika kutenga maeneo ya makazi wakati amwani za makazi ni miundombinu ambayo kwa pamoja inatambulisha mahali halisi mtu ama kitu kilipo, aina hii ya utambulisho inaundwa na vitu vikuu vitatu ambavyo ni namba ya anwani, jina la barabara na postikodi,"alifafanua 


Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Aloyce Mwogofi amesema kikao kazi hicho ni muhimu kwa kuwa kinalenga kujenga uelewa wa pamoja katika kuhamasisha matumizi  ya anwani za makazi na kueleza kuwa wananchi hususani wafanyabiashara wanapaswa kutumia mfumo wa anwani za makazi.


Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mafunzo hayo wamesema kuwa wamefurahishwa kupata elimu hiyo ya anwani ya makazi na kwamba  itawasadia kuinua biashara kutokana na kwamba itakuwa rahisi kutambulika eneo zilipo.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana