Mbunge wa Viti Maalumu kupitia kundi la Wafanyakazi , Dkt Alice Kaijage ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujalimaslahi mbalimbali ya walimu ambapo kwa kipindi kifupi cha uongozi wake mambo yao mengi yameboreshwa. Pamoja na mambo mengine Dkt Kaijage ametoa pongezi hizo alipokaribishwa kuwasalimia walimu wakati wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Disemba 15, 2022.
Dkt Kaijage akiwa na viongozi wengine wakicheza moja ya burudani ukumbini hapo.Mbele yake ni Waziri wa Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Uleamavu, Profesa Joyce Ndalichako.
Dkt Kaijage akirejeA meza kuu . Kulia ni Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt Fatma Maganga
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Kaijage akitoa pongezi zake hizo...
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 0754264203
Post a Comment