Featured

    Featured Posts

RAIS DK. MWINYI ASHUHUDIAUTIAJI SAINI MKATABA NCHINI QATAR, LEO

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameshuhudia leo mchana utiaji saini wa mkataba wa makubaliano ya kuendeleza na kutangaza Zanzibar kama eneo la uwekezaji, biashara na utalii.


Mkurugenzi Mtendaji wa ZIPA, Shariff Ali Shariff, alitia saini kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, huku Bi Elisabete Marques akisaini kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Armasite ya Qatar.


Makubaliano hayo yatachochea ongezeko la wageni Zanzibar, haswa katika sekta ya biashara na usafiri. Aidha, yatasaidia kuimarisha na kutangaza sekta ya utalii Zanzibar kimataifa. Hii inaonyesha dhamira ya Zanzibar kujitokeza kama kitovu cha biashara na utalii katika eneo hilo na kote duniani.


Hatua hii inaunga mkono mpango wa Rais wenye lengo la kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya Zanzibar na Qatar. Sasa, kuna matarajio ya kuona wawekezaji zaidi kutoka Qatar wakiwekeza katika Zanzibar, hatua ambayo itachangia kukuza uchumi wa nchi hiyo.

📆 24 Mei 2023

📍Doha, Qatar

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana