Featured

    Featured Posts

MBUNGE MATHAYO: MICHEZO HUWAEPUSHA VIJANA NA VITENDO VIOVU


 Na Ashrack Miraji, Same Kilimanjaro

Mbunge wa Same Magharibi, DKT David Mathayo amesema  michezo  huwajenga vijana kuwa na mahusiano mazuri Katika nyanja mbalimbali na kuweza kutimiza ndoto zao pia  kuachana na vitendo viovu   kama ukabaji na kutumia madawa ya kulevya, bangi na mirungi. 


Hayo ameyasema wakati akifanya mahojiano na mwandishi maalumu katika kuelekea uzinduzi wa Dkt. Mathayo Cup Novemba 26, 2023 katika Jimbo la Same Magharibi mkoani kilimanjaro ambazo Timu 56 zitakwenda kushiriki mashindo hayo


"Dhamira yangu kwa vijana ni kubwa mno, ni kutaka kuona wanafika mbali na kutimiza ndoto zao hivyo nitakuwa nao bega kwa bega katika kuleta maendeleo chanya kwenye jimbo letu la Same Magharibi kuhakikisha nakuza vipaji vyao,"  alisema Dkt Mathayo.


Dkt Mathayo amesema  pia Mathayo Cup hii ni jitihada za kumuunga mkono Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan  katika sekta za  michezo, tumeona Rais akifuatilia kwa ukaribu michezo  mbalimbali na kuzipa timu zetu  hamasa katika mashindano ya kimataifa na mimi kama muhimu wake katika Jimbo la Same Magharibi nitahakikisha vijana wa Same Magharibi wananufaika Katika michezo na shughuli mbalimbali za kiuchumi.


"Pia nisiwe mchoyo wa fadhira  na niseme ukweli  wa dhati kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amenifanyia makubwa katika jimbo langu, amenijengea vituo vya afya,  barabara   shule  namshukuru sana kwa mchango wake mkubwa hasa kwa wananchi  wa jimbo la Same Magharibi hivyo niwaombe wananchi wa jimbo langu kuendelea kumuunga mkono  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa  kazi kubwa anayoifanya katika kuleta maendeleo kwenye jimbo letu na Taifa."

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana