Na Mwandishi Maalum, TRC
Watumishi watano wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) wamefariki dunia kufuatia ajali ya Treni ya Uokoaji kugongana na Kiberenge No.HDT-3 katika maeneo yaliyopo kati ya stesheni za Mwakinyumbi na Gendagenda, eneo liliilopo katika Reli inayotoka Ruvu Junction mpaka Mruanzi Junction, jana, Machi 22, 2020.
Taarifa ya TRC imewataja waliokufa kuwa ni Ramadhani Gumbo wa DTM Tanga, Injinia Fabiola Moshi wa DME Dar es Salaam, Joseph Komba wa ATM Dar es Salaam, Philip Kajuna -Safety Technical na George Urio - Dereva wa trolley
"Watumishi wa TRC walikuwa sita, Watumishi wanne wamefariki pale pale katika eneo la ajali na majeruhi wawili walifikishwa katika Hospitali ya Magunga ya Wilaya ya Korogwe kwa huduma za Kitabibu.
Mpaka ilipofikia saa 5 usiku Mach 22, 2020 majeruhi mmoja alifariki na kufikia jumla ya watumishi watano waliofariki", imesema taarifa hiyo ya TRC
Taarifa hiyo imesema hadi sasa majeruhi mmoja aliyabaki Elizabeth Bona ambaye in Guard was treni anaendelea na matibabu katika hospitali hiyo.
"Aidha uchunguzi wa kujumuisha taasisi zingine utafanywa kubaini chanzo cha ajali hii hiyo", imesema taarifa hiyo.
Post a Comment