*Anasaidia kusomesha zaidi ya watoto 200 wa kaya masikini.
* Amevipiga tafu vikundi vya kina mama, vijana na wenye ulemavu.
*Mchango wake binafsi umegusa kila sekta Longido.
Na Richard Mwaikenda
MOJA ya kigezo kikubwa ambacho huwa ni kivutio kwa wananchi kumpa kura za ndiyo, mgombea wa kiti cha Ubunge kama anagombea kwa mara nyingine ni namna alivyoweza kujitolea fedha zake binasi katika ujenzi wa miradi ya maendeleo na misaada ya kijamii katika jimbo lake mbali na kutegemea jitihada za serikali.
Mgombea Ubunge Jimbo la Longido kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Steven Lemomo ni miongoni mwa wagombea ambaye anastahili kupigiwa kura za kishindo ili arejee tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo kwa kuwa katika kipindi chake cha miaka mitatu tu ya Ubunge wake, kuanzia 2018 hadi 2020 aliweza kuonyesha ari ya kuchangia maendeleo jimboni ambapo alitumia fedha zake binafsi zaidi ya Sh. Milioni 600 kusaidia ujenzi wa miradi katika sekta mbalimbali na misaada ya kijamii kwa ujumla.
.............................. .............................. .............................. .............................. ..
MKUU huo ni utangulizi tu wa makala yako ambayo endapo tukikubaliana nitaiendeleza kwa kutaja jinsi mchango wako ulivyosaidia kwa kutaja miradi na mambo mengine mengi uliyoyafanya yaliyomo kwenye Taarifa ya yako ya Utekelezaji wa Ilani.
Tunakushauri katika katika kipindi hiki cha lala salama cha kampeni makala yako ichapishwe kwenye moja ya magazeti ilikiwemo la Uhuru halafu ununue kiasi cha nakala za gazeti na kuzisambaza jimboni kwako. Itasaidia sana kuongeza kura zako, za Rais na madiwani..
Post a Comment