Featured

    Featured Posts

VIONGOZI WA NCHI 20, MABALOZI 83 KUHUDHURIA KUAPISHWA KWA RAIS DK MAGUFULI DODOMA

Msemaji Mkuu wa Serikali, Hassan Abbas akizungumza na vyombo vya habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk John Maguuli kwenye Uwanja wa Jamhuri, jijini Dodoma. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA


 Na Richard Mwaikenda, Dodoma

ZAIDI ya viongozi 20 wa mataifa mbalimbali duniani wamethibitisha kuhudhuria kuapishwa kwa Rais Mteule, Dk. John Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Kati ya viongozi hao yupo, Rais wa zamani wa Nigeria, Obasanjo, Rais wa Zimbabwe,  Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Nabii TB Joshua wa Nigeria.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Hassan Abbas alipozungumza na vyombo vya habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya kuapishwa kwa Dk Magufuli kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Abbas amesema kuwa sherehe hizo pia zitahudhuriwa na zaidi ya mabalozi 83 wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Pia sherehe hizo zitanogeshwa na wasanii maarufu nchini wakiwemo akina, Diamond, Ali Kiba, Hamonize, Zuchu, Nandy na wengine wengi.

Milango ya kuingilia uwanjani hapo itafungulia mapema saa 12 asubuhi.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana