Featured

    Featured Posts

RAIS SAMIA ATOA AGIZO KWA GAC NA GAVANA WA BENKI KUU KUPITIA FEDHA ZILIZOTOKA JANUARI HADI MWEZI HUU NA KUTOA TAARIFA ZILIVYOTUMIKA



Dodoma, Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemuagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Dk. Charles Kichere na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenda kupitia fedha zote zilizotoka kuanzia Januari hadi mwezi huu wa Machi ili kutoa taarifa ya kazi zilizofanya.


Ametoa agizo hilo leo Machi 28, 2021 Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma baada ya kupokea taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za mwaka wa fedha 2019/20 na taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2019/2020.


"Naomba nitoe agizo kwako CAG na Gavana wa Benki Kuu yupo hapa, naomba uende ukapitie fedha zote zilizotoka kuanzia Januari hadi mwezi huu wa Machi kwenda kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo, tunataka kuziona,"ameagiza Rais Samia.


"CAG naomba sana ulimi wako usiwe na utata, kama kuna Shirika halifanyi vizuri, tuambie halifanyi vizuri, kama Bodi haisimamii vizuri, tuambie Bodi hii haisimamii vizuri, sababu tutakaposema mapungufu ndio tutakapoweza kurekebisha na tukaweza kufanya vizuri zaidi,"ameeleza Rais Samia.

author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana