Featured

    Featured Posts

WABUNGE, VIONGOZI WANAWAKE WAELEZEA WALIVYOFURAHISHWA NA HOTUBA YA RAIS SAMIA+video

 

Mwenyekiti wa Taasisi ya Matukio ya Wanawake Laki Moja, Rehema Mkuda akielezea furaha yake  jinsi alivyofurahishwa na hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan alipozungumza na wanawake wa Mkoa wa Dodoma kwa niaba ya wanawake nchini kwenye Ukumbi wa Kituo cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma Juni 8,2021.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Singida, Grace Mkoma akifurahia hotuba ya Rais Samia kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam, Janeth Mahawanga akieperusha bendera ya Taifa kwa bashssha wakati Rais Samia akiwahutubia wanawake kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara, Agnes Marwa.



Wabunge wanawake wameelezea jinsi walivyofurahishwa na hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa mkutano na wanawake wa Mkoa wa Dodoma kwa niaba ya wanawake nchini kwenye Ukumbi wa Kituo cha Mkutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma Juni , 2021.

Waliopata wasaa wa kuzungumza na Blog hii ya Taifa ya CCM kuelezea furaha yao hiyo: Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara, Agnes Marwa, Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam, Janeth Mahawanga, Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya CCM Mkoa wa Singida, Grace Mkoma na Mwenyekiti wa Taasisi ya Matukio ya Wanawake laki moja, Rehema Mkuda.

Mdau nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video viongozi hao wakielezea furaha yao hiyo.....

Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
0754264203
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana