Kijana Daud Sostenes maarufu kwa jina la DJ Mkombi ambaye elimu yake ni ya darasa la 7, mkazi wa Wilaya ya Bahi, mkoani Dodoma, ameunda pikipiki ya magurudumu matatu (GUTA) ambayo huitumia katika shughuli mbalimbali ikiwemo kubeba vyombo vyake vya muziki ambavyo hukodiwa na watu mbalimbali zikiwemo taasisi za serikali. Nilipata kufanya mahojiano mafupi na DJ Mkombi juu ya ubunifu huo nilipokutana naye alipokuwa akiendesha shughuli zake za uDJ katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka kusuluhisha mgogoro wa ardhi wilayani Bahi uliofanyika Machi 7, 2022 katika Kata ya Mbamatwa.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
0754264203
Post a Comment