Featured

    Featured Posts

MFUKO WA FEDHA ZA JIMBO - JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

 


Jumatatu, tarehe 16.5.2022, KAMATI YA FEDHA ZA MFUKO WA JIMBO  wa Jimbo la Musoma Vijijini kimefanya KIKAO cha kugawa fedha hizo.


Kikao kimefanyika kwenye Ofisi za Halmashauri yetu (Wilaya ya Musoma, Musoma DC) chini ya Mwenyekiti wake, Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo.


UAMUZI


1. Vifaa vya ujenzi vinunuliwe na Halmashauri yetu na viwe tayari kugawiwa ifikapo Jumatatu ijayo, tarehe 23.5.2022


2. Fedha zilitolewa na Serikali ni Tsh 52.43 million na vifaa vitakavyonunuliwa ni:


Mabati 852 (bando 71)

Saruji Mifuko 596

Nondo 202


SEKONDARI ZILIZOTUMA MAOMBI NI:

1. Kigera    2. Kiriba

3. Mkirira   4. Seka

5. Nyakatende

6. Makojo

7. Nyasaungu (mpya, inajengwa)

8. Murangi      9. Tegeruka

10. Mugango  11. Bulinga


USAFIRISHAJI WA VIFAA VILIVYOGAWIWA


Sekondari iliyogawiwa vifaa vya ujenzi inalo jukumu la kusafirisha, kwa gharama zao, vifaa hivyo.


TAREHE YA MWISHO YA KUTUMIA VIFAA VILIVYOGAWIWA


Ifikapo tarehe 30.7.2022, vifaa vyote vilivyogawiwa lazima viwe vimetumika kama ilivyopangwa. Watakaoshindwa kufanya hivyo, vifaa hivyo vitaondolewa na kupelekwa kwenye Sekondari nyingine  yenye mahitaji ya kuvitumia.


PICHA ya hapa zinaonesha Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo akiwa na  Washiriki wa Kikao cha kugawa Fedha za Mfuko wa Jimbo.


Usisahau kutembelea TOVUTI ya Jimbo letu ambayo ni:

https://ift.tt/DvnNCju


Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

https://ift.tt/DvnNCju



author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana