Featured

    Featured Posts

AFARIKI AKIJIFANYIA UPASUAJI KUPUNGUZA TUMBO

New York, Marekani

Muuguzi mmoja kutokea Nchini Mexico amefariki baada ya kukutwa akiwa amepoteza fahamu katika Ofisi ya Daktari baada ya kujaribu kujifanyia upasuaji wa kupunguza tumbo.


Jarida la The New York Post, limeripoti kuwa Daktari Rolando Samper Mendoza, ambaye ni Mmiliki wa Hospitali hiyo iitwayo ‘Clinica Amper’ ya Mexico amesema Mwanamke huyo alijichoma sindano ya ganzi ili kujifanyia upasuaji huo ambao hana nao ujuzi wala uzoefu wowote. 


Muuguzi huyo alifariki kwa kupata mshtuko wa moyo muda mfupi baada ya kukutwa na Mfanyakazi mwenzake ambaye aliwapa taarifa Wahudumu wa afya na kujaribu kumsaidia.


Mwanamke huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Carina, alijaribu kutekeleza upasuaji huo ili kupunguza tumbo lake Hospitalini hapo, kitendo ambacho kilisababisha Muuguzi huyo kujichoma kiasi kikubwa cha ganzi ambayo ilimsababishia madhara.



author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana