Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Komredi Godfrey Daniel Chongolo, leo Oktoba 18, 2023, amekagua utekelezaji wa ujenzi wa mji mpya wa Serikali Mtumba kwa yeye na baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taifa kutembelea jengo la Wizara ya Maliasili na Utalii ambalo Ujenzi wake umekamilika.
Akizungumza mara baada ya kuupokea ujumbe huo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi, alisema pamoja na kukamilika jengo hilo pia limeshafungwa vifaa vya kisasa vya mawasiliano na usalama wa jengo na wakati wowote wataanza kulitumia.
Post a Comment