Featured

    Featured Posts

UZINDUZI WA JIMBO AICT KITANGILI SHINYANGA

 HISTORIA YA  JIMBO AICT KITANGILI -DAYOSISI YA SHINYANGA 

Viongozi wandamizi Kanisa la AIC Jimbo la Kitangili Shinyanga


Mnamo Septemba 08-10, 2021 Baraza la Sinodi kuu,Buzuruga,Mwanza lilipitisha Katiba iliyorekebishwa kukubali mabadiliko ya kiuendeshaji ikiwemo Kubadili jina la ngazi ya Chalo kuwa Jimbo basi,mnamo tarehe 14/05/2022 ndipo Jimbo la AICT Kitangili likanzishwa likiwa na Pastoreti 12, Wachungaji 13, Wainjilisti 53 na Kanisa za mtaa 53.kama ifuatavyo

  1. Pastoreti  8 zimo katika Manispaa ya Shinyanga ambazo ni: Kambarage,Mlima Betheli -Kitangili,Ndala,Nhelegani,Giligali – Ngokolo, Samaria-Bugweto,Chibe na Old Shinyanga.
  2. Pastoreti 2 zimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambazo ni: Mishepo na Usule.
  3. Pastoreti 2 zimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambazo ni: Bethelehemu- Bunambiyu na Bulima.
Sherehe ya kuwavika mataji viongozi wadamizi zilikuwa zimefana

BARAZA LA KWANZA LA JIMBO

 Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga Zakayo E.Bugota mnamo tarehe 14/05/2023 alisimamia Baraza la kwanza la Jimbo AICT Ktangili kufanya mambo yafuatayo

Kuchagua viongozi  Wandamizi wa Jimbo kama ifuatavyo:

  • Mchungaji Paul Makenzi Kidanha kuwa Mchungaji Mwenyekiti wa Jimbo
  • Mchungaji Joshua S.Masaga kuwa Mchungaji Mwenyekiti Msaidizi wa Jimbo.
  • Mwalimu Samwel Lazaro Maziku kuwa Kaimu Katibu wa Jimbo na
  • Mwinjilisti Anna Charles Lugenji kuwa Kaimu Mhasibu wa Jimbo.
Viongozi wandamizi wakisimikwa 14/05/2023

Kuamua kuwa Makao Makuu ya Jimbo la Kitangili yawe  Pastoreti ya Mlima Betheli-Kitangili.

Sherehe ya kuwapongeza viongozi wapya wa AICT Jimbo la Kitangili Shinyanga

Ibada Maalumu ya  uzinduzi wa Jimbo la AICT KITANGILI  ilifanyika Oktoba 15 Jumapili 2023 ikiongozwa na Baba Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota kwa:-

  • Kuzindua Jimbo
  • Kusimika viongozi wandamizi wa Jimbo na
  • Kusimamia mchango wa Ujenzi wa ofisi za Jimbo


author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana