Featured

    Featured Posts

WADAU WA HABARI WAJITOKEZA KUTOA MAONI KAMATI YA KUTATHMINI HALI YA UCHUMI WA VYOMBO VYA HABARI

Baadhi ya wadau wa habari wakiwa katika kikao cha kutoa maoni kuhusu tathmini ya hali ya uchumi wa vyombo vya habari na wanahabari mbele ya wataalam na wajumbe wa Kamati iliyoundwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekonolojia ya Habari, Nape Nnauye kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari jijini Dar es Salaam Novemba Mosi, 2023.

Waliotoa maoni yao  siku hiyo ni kutoka: Jumuiya ya Wanahabari ya Mitandao ya Kijamii Tanzania (JUMIKITA), Global Online TV, Ayo TV na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Wanaotakiwa kujitokeza  kutoa maoni kesho Ijumaa Novemba 3, 2023 ni: Taasisi za ndani  za vyombo vya habari  na wasimamizi wa sekta: Baraza la Habari Tanzania (MCT),  Umoja wa Kalabu za Habari za Mikoa Tanzania (UTPC), Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA),MISA-TAN, TMF na KADIO.

Aidha, kamati imeanza awamu ya pili ya kusambaza madodoso juu ya suala hilo yanayotakiwa kujazwa na waandishi wa habari pamoja na wafanyakazi walio kwenye vyombo vya habari.

Kamati iliyopewa jukumu hilo ina wajumbe wafuatao: Tido Mhando (Mwenyekiti), Dkt. Rose Reuben (Makamu Mwenyekiti), Mobhare Matinyi (Katibu), Sebastian Maganga, Richard Mwaikenda, Bakar Machumu, Joyce Mhavile, Kenneth Simbaya na Jacqueline Woiso. 


Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile (kushoto) akitoa maoni kwa niaba ya jukwa hilo.Kulia ni Mtaalam kiongozi wa kamati hiyo, Abdallah Katunzi.











 
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana