Mwandishi Maalum, Dar es Salaam
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema kuna haja na umuhimu wa kuwa na vituo vya kutoa huduma ya pamoja ( One Stop Center) kwa waahiriwa wa matukio ya ubakaji na uyanyasaji wa kingono.
AG Jaji Dk. Feleshi ametoa ushauri huo mwishoni mwa wiki alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Legal Service Facility (LSF) Lulu Ng’wanakilala, Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Amesema uwepo wa vituo hivyo si tu utaongeza kasi ya kushugulikia matukio hayo lakini pia utaharakisha upatikanaji wa haki kwa wakati na kutoa ahueni kwa waathiriwa wa matukio hayo.
AG Jaji Feleshi ameishauri Taasisi hiyo ya LSF ambayo ni mdau muhumu kulifanyia kazi suala hilo kwa kushirikiana na wadau wengine nje ya Serikali kwa kile alichosema kwa sababu wao tayari wanazo pragramu kadhaa wanazoshirikiana na Serikali.
Aametolea mfano wa Nchi ya Afrika Kusini ambayo imeazisha vituo kama hivyo vinavyojulikana kama Thuthuzela Care Center na kwamba uwepo wa vituo hivyo ambavyo vimesambaa katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo umerahisisha sana ushughulikiaji wa matukio hayo na utoaji wa haki kwa wakati.
Akifafanua zaidi kuhusu vituo hivyo , AG jaji Feleshi, amesema vituo hivyo vitatakiwa kuwa na watoa huduma wenye utaalamu na weledi wa kushughulikia visa hivyo.
“Vituo hivi vinatakiwa kuwa na daktari, Polisi, mpelelezi, Mwendesha Mashtaka, Afisa Ustawi wa Iamii, Wataalamu wa Saikolojia na Ushauri Nasaha pamoja na wadau wengine.
Inatakiwa muathiwa aliye nyanyaswa kingono au kubakwa anapofika kituoni hapo anapate huduma zote hapo hapo, kama daktari anakuwapo, kama mpelelezi yupo, kama mwendesha mashataka anakuwapo na polisi anakuwapo”. Anabainisha AG Jaji Feleshi.
AG Jaji Feleshi amebainisha kwamba, kwa uzoefu wake akiwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali lakini pia kama Jaji amekuwa akishughulikia kesi za ubakaji na unyanyasi na kushuhudia mashauri mengi kutofikia tamati kutoka na sababu nyingi zikiwamo za upepelezi na ushahidi kuvurugwa.
“Wakati mwingine unaona kabisa hapa kuna kesi ya kujibu na haki inatakiwa kutendeka lakini mara unakuta mpelelezi anashindwa kuifanya kazi yake ipasavyo au ndugu wa muathiwa wanaingilia kati kwa kutaka wayamalize kifamilia, kimilia au kwa kuficha ushahidi na hata kumrubuni muathiwa", Amebainisha AG Jaji Feleshi.
Akasema, jambo lingine linachangia kutopatikana kwa ushahidi wa kumtia mtuhumiwa hatiani ni kwa waathiriwa kutoenda Polisi mapema baada ya tukio au wanakwenda Polisi wakati ushahidi umeshavurugwa.
“Sheria inataka muathiwa anapofanyiwa uovu huo aende mara moja Kituo cha Polisi au Kituo cha matibabu, lakini hali ilivyo ama waathika wengi wanaficha uovu huo kwa sababu mbalimbali au wanakwenda kutoa taarifa wakati ushahidi umeshavurugwa, Napenda kusisitiza kwamba, kuficha kosa ni kosa kisheria” amesisitiza.
Anasema matukio ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono ni 'very technical' katika kuyashughulikia kutoka na mazingira na unyeti wa matuko yenyewe na ndiyo maana uwepo wa vituo hivi utasaidia sana kwa sababu wataalamu wote watakuwa mahali pamoja.
AG Jaji Feleshi amesema pamoja na uwepo wa madawati ya jinsia katika vituo vya Polisi na uwepo wa mashirikia yasiyo ya kiserikali yanoshughulia matukio hayo bado jitihada zaidi zinahitajika.
Akasema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka tayari yana Divisheni zinazoshughulika na masuala ya Uratibu hivyo Ofisi hizo mbili zitakuwa tayari kutoa ushirikiano katika jambo hilo.
Kwa upande wake Mkurugenzi huyo wa LSF amemshukukuru Mwanasheria Mkuu kwa wazo hilo na kwamba watalifanyia kazi na kwamba Taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine katika utoaji wa msaada wa kisheria pamoja na kuwaelimisha na kuwawezesha wadau wao hususani wanawake kuhusu masuala yahusuyo sheria pamoja na kutambua haki zao.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Dk. Eliezer Feleshi akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Service Facility. Lulu Ng'wanakilala, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika mwishoni mwa wiki ofisni kwake Jijini Dar es Salaam. (Na Mpihapicha Maalum)
Post a Comment