Katika kikao hicho, Chongolo akisikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi ikiwemo ujenzi wa bwawa kwa ajili ya maji ambapo aliagiza ujenzi wake uanze Juni 10, 2023, kuwapelekea umeme ambapo meneja wa Kanda wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA), akiahidi kuwa jambo Hilo litakamilika Desemba mwaka huu.
Aidha, ameiagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohammed Mchengerwa anaharakisha ulipaji fidia kwa walioathirika kwa namna moja ama nyingine na wanyamapori wanaotoka hifadhi ya Mkungunero.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM, Sophia Mjema akihutubia katika kikao hicho kwa kuwataka Wazazi kuwapeleka Shule watoto wa kike badala ya kuwaozesha na kuwatafutia ajira za majumbani.
Mwenyekiti wa Shina namba 6 Itaswi Kondoa Vijijini, Msafiri Steven akifunga kikao hicho. Kulia ni Komredi Chongolo.
Post a Comment