Featured

    Featured Posts

PSSSF YAVIPIGA JEKI VITUO VYA AFYA KATAVI NA MTWARA

*Ni katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma.

NA K-VIS BLOG

Vituo vya Afya vya Ilembo, Mpanda na Ikombe Mtwara vimepatiwa msaada wa Vifaa tiba kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumisjhi wa Umma (PSSSF) ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma iliyoanza Juni 16 na kilele chake ni Juni 23, 2023.

Misaada hiyo ni njia ya kuthamini mchango mkubwa wa watumishi wa umma katika kuleta maendeleo na ustawi katika jamii lakini pia kuunga mkono juhudin za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongoze wake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuboresha huduma za Afya maeneo mbalimbali nchini, Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbarouk Magawa alisema wakati akikabidhi vifaa tiba Kituo cha Afya Ikombe, nje kidogo ya Manispaa ya Mtwara.

“Mnafahamu tuko kwenye Wiki ya Utumishi wa Umma kama Mfuko huwa tuna utaratibu kwa viongozi walioko Makao Makuu kupita kwenye ofisi za mfuko zilizoko pembezoni mwa nchi ili kujadiliana changamoto mbalimbali zilizopo na namna ya kuzishughulikia, lakini pia tunao wajibu wa kusaidia jamii inayozunguka ofisi zetu na ndiyo maana tuko hapa leo.” Alisema.

Alisema msaada huo ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya nchini, hivyo kile kidogo tulicho nacho kama mfuko tumeona tuwaunge mkono.” Alifafanua

Naye Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, PSSSF Bw. Paul Kijazi ambaye yeye alikabidhi vifaa tiba kwenye Kituo cha Afya Ilembo, kilichoko mjini Mpanda, Katavi, alisema Mfuko umekuwa na utaratibu wa kuchangia kiasi kinachowezekana kwa mujibu wa bajeti yake.

“Tunatambua umuhimu na uzito wa kazi mnazofanya kama kituo cha afya lakini ninyi ni wanachama wa PSSSF, bila ya ninyi sisi hatupo, lakini pia mnahudumia jamii na sisi kama taasisi inao wajibu wa kutambua jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali katika kuboresha huduma kwa wananchi.” Alisema Kijazi.

“Tunafahamu kuna changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa utoaji wa huduma ikiwemo huduma za afya, na pale ambapo Mfuko unaona unaweza kuchangia kwa kiasi kinachowezekana kwa mujibu wa bajeti umekuwa ukifanya hivyo katika makundi na taasisi mbalimbali.

Katika kipindi hiki cha Wiki ya Utumishi wa Umma, tumeteua baadhi ya sehemu kwa uwezo wetu kama Mfuko tumeona tuweze kuchangia kidogo kilichopo ili kiwawezeshe ninyi muweze kufanya akzi zenu vizuri na wananchi nao wapate huduma bora.

Wakitoa shukrani kwa nyakati tofauti baada ya kupokea misaada Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ilembo, Dkt.Limbu Mazoya aliishukuru PSSSF kwa msaada huo.

“Vifaa hivi vitasaidia kupunguza changamoto zilizokuwepo, tulikuwa tunakabiliwa na upungufu wa baadhi ya vifaa na kwaweli vitatusaidia sana na kupanua wigo wa watu tunowahudumia.” Alisema Dkt. Mazoya.

Naye Muuguzi wa Kituo cha Afya Ikombe, Lilian Mlaponi alisema moja ya mahitaji makubwa ambayo kituo kilikuwa kinahitaji ni pamoja na mashuka na hivyo msaada huo utasaidia wagonjwa watakaokuwa wanalazwa kwenye kituo hiocho.” Alisema.



Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbarouk Magawa (wapili kushoto) akikabidhi sehemu ya misaada hiyo kwa uongozi wa Kituo cha Afya Ikombe kilichoko nje kidogo ya Manispaa ya mji wa Mtwara Juni 22, 2023.



Mkurugenzi wa Rasilimali Watu PSSSF, Bw. Paul Kijazi (watatu kushoto) akiwa na Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa Mfuko huo, Bw. Ramadhan Mgaya (wapili kushoto) wakikaboidhi sehemu ya misaada hiyo kwa uongozi wa Kituo cha Afya Ilembo kilichoko Mpanda Mkoani Katavi Juni 22, 2023.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu PSSSF, Bw. Paul Kijazi (watatu kushoto) akiwa na Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa Mfuko huo, Bw. Ramadhan Mgaya (wakwanza kushoto) wakikaboidhi sehemu ya misaada hiyo kwa uongozi wa Kituo cha Afya Ilembo kilichoko Mpanda Mkoani Katavi Juni 22, 2023.
Bw. Kijazi akizungumza.
Meneja wa PSSSF, Mkoa wa Katavi, Bw. Paul Mbijima (aliyesimama) akizunguzma mwanzoni mwa hafla hiyo.
Bw. Kijazi akikaribishwa na Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ikombe, Dkt.Limbu Mazoya 



author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

www.CodeNirvana.in

Magazeti Ya Leo

Copyright © Magazeti ya Leo, Habari Leo Tanzania, Mwananchi, Michuzi, mwanaspoti, nipashe, Udaku | Designed By Code Nirvana