Akizungumza katika kikao hicho na kusikiliza kero zao, Komredi Chongolo ametoa ahadi ya kwenda kumueleza Rais Samia Suluhu Hassan Ili kuitafutia ufumbuzi changamoto ya maji katika Mji wa Namanyere Ili ibaki kuwa historia.
Aidha ameiagiza Wakala wa Umeme Vijijini REA kuhakikisha wanakamilisha haraka usambazaji wa Umeme katika vijiji vichache vilivyobakia wilayani Nkasi.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa, Bupe Mwakang'ata (kushoto), akiwa katika kikao hicho.
Mwenyekiti wa Shina hilo, Shoma akifungua kikao.
Mbunge wa Nkasi Kusini, Mbogo akielezea kero mbalimbali zinazoikabili Wilaya ya Nkasi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Makongoro Nyerere akizungumza wakati wa kikao hicho.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
Post a Comment